[.:ENGLISH:.|.:ITALIAN:.|.:FRENCH:.|.:SWAHILLI:.|.:HINDI:.    
 
 


 

News letter subscription
   
Name
Email
 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

KUNYAKULIWA NA KUINGIA KATIKA UPENDO

PDF

 

1 Wathesalonike 4:16-18.

16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17 Kisha sisi tulio hali tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili kumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa na Bwana milele.

18 Basi farijianeni kwa maneno haya.

Na hivyo tutakuwa na Bwana milele...katika ulimwengu uliosongeka kwa shida na matatizo, isikize sauti yake Mfariji aliye ndani na ukafarijike kuhusu tumaini hili lililobarikiwa. Tumaini hili nalo ni la kuungamanika naye Bwana, muumba wa mbingu na dunia. Bwana ndiye Roho anayejikusanyia mataifa yote ya ulimwengu ambayo yamekitwa katika giza na upumbavu. Yeyote asikiaye na kusadiki ule mwito wa kuungamanika naye Bwana ni Roho mmoja naye Bwana, kumaanisha kuwa sio wawili tena, kwa sababu ule ukuta uliodhaniwa na fikra zao kuwa uliwatenga haupo tena na Mungu anafanyika yote ndani ya yote. Basi tutaungamanika na Bwana milele...kumaanisha kuwa kifo hakimo tena, kwa sababu kama aishivyo uhai milele, hata sisi twaishi vile vile.

Furahini!!! Nami nasema furahini, mnapoisiskia habari hii njema inayotiririka kutoka Sayuni. Iweke hofu na huzuni mbali. Yabadilishe mavazi yako meusi ya huzuni na kuomboleza ukayavae mavazi tukufu ya sifa. Macho yako yakilenga milima idumuyo milele, ukafurahi kwa ajili ya Neema hii isiyoelezeka iwanyanyuwao wanadamu kutoka masagio makali ya kifo na kuwakusanya katika ushirika wa kweli wa upendo katika wingu lile la utukufu. Yote ni kuhusu Ushirika wa Upendo na furaha ya milele katika mahali pa mbingu, ambamo wote waishi kwa ajili yake Bwana pekee wakitazama uzuri wa Maumbile Yake. Huu ukweli unalinganishwa na Yerusalemu mpya inayoshuka kutoka mbinguni, maumbile Yake Mungu yanayoingia mahali ambamo yanawezaonekana. Mkashukuru na kufurahia. Tena nasema furahini.

Kama umeamka kwa kiwango fulani, utajua ya kuwa usiku waisha na bambazuko laja, nuru ya asubuhi yaingia. Nuru kuu ya ufunuo yang'aa kumfunua Mungu wa ukweli Aliye Baba wa Upendo Aliye kati ya kila mwanadamu. Wale wanafunzi walioitambua na kuifuata ile Nuru waliieneza ile habari njema na kutangaza kuwa "Mungu Ni Upendo". Ndani mwao, Nuru hii iliyo safi ilikuwa imeangamiza kila uongo uliokuweko uliosema kuwa Mungu ni wa ghadhabu na wa kujilipishia kisasi, na asiyetulizwa na lolote isispokuwa jicho kwa jicho na jino kwa jino.

Katika upumbavu wake na kujikaza kwake kidini, Paulo aliondoka na kuanza maangamizi yake, kwaangamiza wale waliojaribu kuenenda dhidi ya sheria za juu juu zilizoitwa za Musa walipomkiri Kristo. Na angefanya lipi lingine kama aliowaiga ni Musa na Eliya na Daudi, ambao wenyewe walieneza maangamizi kupitia kile walichokiona kuwa mtazamo wao kumhusu Mungu. Hawa watu walikuwa na nia nzuri, na walifanya walichojua kulingana na nuru chache waliokuwa nayo. Lakini Yesu ambaye ndiye Nuru Dhahiri yake Mungu baadaye alikiri kuwa "Nuru iliyoko ndani mwako ikiwa ni giza, basi una giza kuu kivipi!" Wakati Nuru ya Kweli ilipomkabili Paulo akielekea Dameski,yeye alikiri ya kuwa Mungu ni Upendo. Alikiri kuwa Mungu Ni Mmoja na ni yote ndani ya yote. Aliiona Nuru ya Ulimwengu.

Mungu Ni Upendo na Ule Upendo wajaza kila kitu. Hakuna kinachopinga hili ndani ya mioyo ya wanadamu kinawezastahimili Nuru ya Ufunuo huu unaofunuliwa na kung'aa sasa. Huu ufunuo unaong'aa kutoka vilindi vyake Baba, ndio lile Ziwa La Moto maarufu linalozikabili kifo na mauti, ambamo ndimo makao mwa uongo wote na mahali ambapo mwanadamu ameweka malazi yake katika maasi yake. Nuru yake nyeupe na miale isiyoonekana kwa macho ya wanadamu, yaangamiza kila fikra na wazo katika njia Yake lipingalo Upendo, Upendo ambao ndio kina na moyo wa kila kitu kilichoko. Upendo wabaki kuwa chanzo na mwisho wa kila kitu. Upendo ndio Ile Nguvu iliyositirika na isiyoonekana kwa macho ya wanadamu, izilishazo na kuzihifadhi sayari na limwengu lizoko.

Hata ingawa haijulikani, na mara nyingi hupuuzwa na wengi kimakusudi, ambao wamesongwa na mizigo ya maisha wanayoishi sasa, fani tofauti za huu Upendo zaonekana dhahiri, zikionekana kupitia mambo yaliyoumbwa. Tukilitafakari jambo hili kuu na la kushangaza, mwanadamu lazima ajifunze kutoka mifano ya Nuhu, Henoko, Musa na Eliya na wengine wengi waliofunguliwa kutoka vifungo vinavyowafunga wengi ulimwenguni tunaoishi na kuingia kwenye utulivu ambamo sauti yake mwanadamu huisha na kubakia ikisikika Sauti yake Mungu pekee. Mwanadamu lazima aelewe kuwa alitoka mahali hapa patulivu akiwa pweke na uchi, na itambidi ayaachiliye yote ili kurejea kule ambako vazi lake pekee ni Upendo.

Tukinena kwa mfano, Nuhu aliyaacha yote ulimwenguni na kukwea vilele vya Sayuni na kuvumbua mbingu mpya na nchi mpya ambamo Upendo, uambatanifu na haki ya Ukweli zapatikana. Henoko aliishi maisha yake kwanza kwanza kama mwanadamu wa mwili na nyama. Lakini aliyaacha yale na kutembea naye Mungu kumaanisha kutembea naye Roho pweke. Mwali wa moto wa Upendo ungemmeza yeye hatimaye, asijepatikana. Musa akakwea na kuuwacha utukufu wa Misri, ambayo ni ishara ya mwili na damu na kuupata Uwepo wa Milele uliofichika nyuma ya vinavyoonekana. Alivumilia makali ya jangwa na miiba yake, majoka, ngee na mbweha wakali, ambazo zinaashiria kutoamini kunakotokana na fikra na mawazo ya kiwanadamu. Kwa kuendelea kwake na kuvumilia, alikutana na Ule Mwali wa moto wa Upendo kwenye kilele cha ule mlima Uliotangaza Ukweli wa Mungu Aliye mmoja na Aliye ndani ya kina cha kila kitu.

Uwache Upako wa ndani ukakuelekeze mahali pale patulivu. Lisikusumbue wala kukushawishi vingine lolote lile. Usiondolewe kutoka safari hii ya kuutambua Upendo katika vilele vyake Mungu. Njiani mle, msafiri anayeutafuta Ukweli itambidi asiangalie nyuma kama alivyofanya mkewe Lutu akafanyika nguzo la chumvi ambayo ni ishara ya mauti na utasa katika maarifa yake Mungu.

Suluhu linalosalia kwake mwanadamu, ni kuyaondoa mawazo yake kwa mambo ya ulimwengu huu tulio, na kutojaribu tena kuhifadhi lolote lile kwenye 'mema' yake, bali kuachilia vyote kwa ajili ya Upendo. Ni kuwaacha ndugu, mashamba, nyumba za kifahari, na nia zote zake mwanadamu ziambatanazo na ulimwengu tulio sasa, tukiwa na ahadi dhabiti kuwa yote haya hurejeshwa mara mia kwa mia katika Milki ya Mbingu ya Upendo. Na uyaache ya kale ya kilimwengu yapite na mapya ya Upendo wa kimbingu uwepo.

Katika hali hii yako mpya ya utulivu, tafakari kwa macho yako ya ndani na utaona kuwa yote yanayodhihirika kwenye ulimwengu huu tulio ni fumbo tu linaloimba ule wimbo wa Upendo na Utukufu wa Ufalme wake Baba usioonekana. Wimbo huu waelezea Utukufu, Ukuu na Milki ya Mungu aishiye. Wafunua Upendo usioelezeka, na Umoja uliopo...kutotengeka kwake mwanadamu naye Mungu aishiye. Katika sauti tofauti za zumari na kinubi, walioamka wasikia mstari huu wa wimbo..."...Mimi ndimi Bwana, na kando Yangu hamna mwengine." Na "Dunia imejaa Utukufu wake..."     Angalia vilindi vya nchi na sayare na nyota, na utaona ni wingi wa Upendo unaojidhihirisha kwa njia nyingi na tofauti.

Ukweli huu wadhihirishwa bayana katika kichwa cha wimbo huu "Milima Ii Hai" katika sinema iliyotia fora sana iitwayo "Sauti Ya Muziki".

MILIMA II HAI

Milima ii hai na sauti ya mziki

Ikiwa na nyimbo zilizoimbwa miaka maelfu

Milima yajaza moyo wangu na sauti za mziki

Moyo wangu wataka kuimba kila wimbo usikiao.

Wakati Richard Rogers aliuunda ule wimbo wa ile sinema "Sauti Ya Wimbo", hakujua alikuwa anaingia kwenye mashina na vilindi vyake Mungu. Bila ya kujua, mtunzi huyu alinena kuhusu Ukweli ulio wa jadi katika Milki yake Mungu. Miaka elfu (karne) katika milima inaashiria Milki yake Mungu ambayo yajulikana pia kama Siku Ya Bwana. Milima ya milele ya Sayuni ii hai na sauti za nyimbo, na kila mmoja aishiye kwenye ule mlima amejihami kwa kinubi cha dhahabu wakipiga wimbo maridadi wa kumtukuza Aishiye milele. (Ufunuo 1:1-3). Ule umaridadi wa wimbo unafananishwa na ule wa wana wa Mungu, wale nyota wa asubuhi wanaotajwa kwenye vyuo vile vya kale vya Ayubu, walioimba kwa furaha na kwa pamoja wakati misingi ya ulimwengu ilipowekwa (Ayubu 38:4-7).

Ikisomwa tu kwa mawazo ya kiwanadamu, Ayubu 38 yaonekana kana kwamba ni hadithi tu ya kihistoria, lakini sio vile hasha. Inafunua Ukweli uliopo hata kupita muda na wakati...ushirika wa kiungu unaomiliki na kutawala katika Mungu mbinguni. Wawezaliita Kanisa la Mzaliwa wa Kwanza ama Kusanyiko lake Mwenye Nguvu Sayuni. Hii ndiyo nguvu ya limwengu zote. Kama huu Ushirika wa Upendo kwenye vilele vyake Mungu haungekuweko, hakuna kitu kilichoko kingekuwa. Ni kweli mbingu zatangaza Utukufu wake Mungu.

Zaburi 19:1-4.

1 Mbingu zahubiri Utukufu wake Mungu, na anga laitangaza kazi ya mikono yake.

2 Mchana husemezana na mchana, usiku hutolea usiku maarifa.

3 Hakuna lugha wala maneno, Sauti yao haisikilikani.

4 Sauti yao yaenea duniani mwote, Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu. Katika hizo ameliwekea jua hema.

Katika andiko hili, mbingu zaashiria kusanyiko la wana wa Mungu, nyota za asubuhi au malaika wote wakitangaza makuu ya Utukufu wake Mungu. Na haya yote ni katika mambo yanayoonekana. Kilele cha uhusiano huu wa mapenzi na kuabudu katika mbingu, vitu vilivyoumbwa hutokea na kuonekana. Nguvu za Upendo katika kusanyiko hili huumba na kuzihifadhi chembe zote zifanyazo sayare, nyota na ulimwengu mzima.

Ni kweli inayotambulika kuwa Mungu alizifanya mbingu na dunia na kila kitu kupitia mtu mmoja wa kimbingu tumwitaye kwetu sisi Kristo. Lakini kweli hii sio kamili usipotambua kuwa wewe ulikuwa ndani mwake kabla ya misingi ya ulimwengu, na kabla ya kitu chochote kudhihirika. (Yohana 15:27). Inamaanisha kuwa mwanadamu umwonaye akitembea pembeni alikuwa Roho Moja na Bwana kabla ya kushushwa kwake katika huu mwili unaojihisi kuwa umetangwa na Mungu. Ulikuwa ndani yake kabla ya ujuzi huu tuuitao ulimwengu wa mwili na damu. Ulikuwa ndani Yake kabla ya kufanyika chini ya malaika au wana wa Mungu katika ulimwengu tulio. Ulimwengu tulio ni matunda tu ya upumbavu na kutoelewa kuwa mwanadamu amekitwa katika Uhai Mmoja Wake Mungu na ndio Kristo. Wewe ni Muumbaji pamoja na Mungu katika Kristo. Wewe ni Kazi yake kwa kweli. Hili linatuondolea hekaya tulizoziamini kuwa Kristo ako mahali fulani kule nje amejitenga nasi. Kristo ndio ule Mwili wa Mbingu ambao ndani Mwake ni kusanyiko lisilohesabika la jeshi la Mbinguni. Hiki ndicho chanzo chake mwanadamu katika Utukufu.

Kuungamanika huku kwa mwanadamu na Mungu kwaonekana katika wimbo ule wa mapenzi unaodhihirishwa kama mti na matawi yake, ama mwili na viungo vyake. Bila matawi, mti haupo. Na bila viungo, mwili haumo. Sayare na nyota kule juu zadhihirisha kusanyiko hili la kilimwengu katika vilele vya Nguvu na Milki yote mbali na kupita vikwazo vya muda na wakati.

Mambo kama haya yawezasikika kama hekaya na hadithi tu kwa yule anayesikia, ambaye amezoea kusongeka na vilivyo vinyonge na vidhaifu vya ulimwengu wake mwanadamu wa mwili na nyama. Lakini kila mtu aamrishwa kutega sikio ili kusikia na kumruhusu Roho Tulivu kumwongoza tena kwenye mahali pake katika Huu Mwili. Nuru ya Ufunuo yang'aa tena leo ili kumwamsha mwanadamu katika Ukweli kuwa YEYE NI KIUNGO MUHIMU KATIKA KRISTO, AMBAYE NDIYE MWILI WAKE MUNGU. Upumbavu uliopo kulihusu hili jambo hakuwezi kulifutilia mbali. Ni Kweli na ya kudumu. Baba awakumbusha wanawe kuhusu vilele walivyoanguka kutoka, na atafuta njia ya kuwarejesha katika hali tukufu ya wanawe Mungu na nyota za asubuhi walizo. (Ufunuo 2:5).

Imenakiliwa kimakusudi kuwa pale mwanzo, katika maumbile yake Mungu, nyota wa asubuhi WALIIMBA PAMOJA na wana wake Mungu walishangilia wote kwa furaha. Roho wake Mungu afunua Umoja na Upendo ulioko katika Roho. Kwa kweli, ni vyema kiwango kipi ndugu wakiwa pamoja katika Umoja. Upako wa uzima humiminika kwao, amani na furaha bila kipimo (Zaburi 133). Umoja huo mkamilifu hupatikana tu kwenye vilele vya Sayuni, Milki iliyoinuka ambamo ndio makaazi yake Mungu na huko ndiko kunakosalia tumaini lake mwanadamu ambaye anawezapambanua Kweli leo. Katika mahali hapa palipoinuka, mwanadamu huishi kupitia Kweli katika hisia zilizoinuka mahali ambapo ataona na kutembea tu katika uhusiano na Mungu na Ufalme wake pekee. Ili kuufikia Utukufu huu uliomkwepa mwanadamu, lazima ajizoeshe katika Kweli na akaweze tena kujuana na mambo yasiyoonekana yake Mungu. Mambo haya ya Mungu ni ya kutoonekana tu kwa muda. Mwanadamu anapoamka kikamilifu katika hisia zake ndani, yaliyoonekana kuwa siri zake Mungu yatafanyika ufunuo bayana.

Yeye asema, "Nitaja niwakusanye, ili NILIPO nanyi pia muwe" (Yohana 14:3). Huku ni kule kuyakusanya mataifa yaliyotawanyika na kuyafanya Moja, ambalo ni Kristo. Ndiko kule kukusanya kusanyiko la zile nyota za asubuhi na wana wa Mungu Mlimani Sayuni, mahali palipoinuka, makaazi yake Mungu. Mataifa yote yatatiririka hadi vilele vya Sayuni na yaungamanike tena na kuwa Mmoja na Kristo. Hili limezungumziwa sana kuhusu kurejea kwao waliokombolewa Mlimani Sayuni. Katika kuungamanika huku kwa kiungu, kunao ule Uzima na Nguvu ziumbazo na kuhifadhi kila kilichoko.

Na kwa wengi walioupata huu ufunuo wa Kristo, amewafanya kuwa wana wake Mungu na kwa hiyo wamepata unjia wa kuingia katika lile kusanyiko la wote katika Mwana (Yohana 1:12). Roho pia asema, "yeyote ashindaye nitampa ile nyota ya asubuhi" (Ufunuo 2:26-28). Kwa maneno mengine, ashindaye uogo wa shetani kuwa yeye ametengwa na Uzima na Utukufu wake Mungu, nitampa nyota ya asubuhi ili akang'ae tena katika Utukufu kama jua ling'aavyo. Matendo tofauti yake Roho wake Mungu kati yetu leo, yasaka kutukusanya wote turejee katika Umoja wa Imani vileleni mwake Mungu, mahali ambapo Uwepo wake na Baraka zake zisizo kipimo huishi.

Kwa muda mchache, Yesu angefunua hii Milki ya ushirika wa Mbingu kwa wafuasi wake watatu alipobadilishwa mlimani fulani uliotengwa. Ili kufika pale, iliwabidi wasafiri siku tatu wakipitia njia milimani zenye ukiwa na mawe makuu. Na zile njia zaashiria mapito yake yeye anayerejea palipo patulivu. Walipofika pale, macho yao kwa muda yalifunuliwa kuona Milki isiyoonekana yake Mungu na Uzuri wake. Dhibitisho la hili laonekana kupitia yule mfuasi aliyetamani sana kubakia pale baada ya kuonja furaha na Utukufu wa Uwepo wake Mungu. Kwa kweli hakuna awezaye kuuonja Uwepo wake Mungu na kusalia alivyo. Kileleni mwa mlima ule, walimezwa na kufunikwa kwa wingu lenye Nuru ya Utukufu, na kutoka kwalo sauti ikaguruma na kukiri, "Huyu ndiye Mwanangu mpendwa, msikieni yeye".

Sadiki kuwa, waliona onyesho dhahiri la kusanyiko nzima la watakatifu au wana wa Mungu katika Nuru. Lile wingu lenye Nuru ya Utukufu sio lingine bali ni lile Wingu la Mashahidi walioungamanika na kuwa Mmoja na Baba. Mwana wa Mungu alikuja kufunua hii Milki kwao wanadamu na kuwakusanya wao kurejea katika Ushirika huu. Hii ndio siri ya Ushirika uliofichika katika Mungu kabla ya misingi ya ulimwengu lakini sasa yawekwa dhahiri kupitia Injili (Waefeso 3:8-9). Ni Ushirika mtakatifu wa Upendo na Umoja wake Baba na Mwana (1 Yohana 1:13). Na ni vyema kwako kutambua kuwa hiki ndicho chanzo chako wewe. Awaye yeyote yule anapotambua chanzo chake ndani yake Mungu, pale pale atajua Mwisho. Kwa sababu Ufunuo huu ndio Nuru ya kukufungua wewe kutoka kwenye vifungo vyake yule muovu.

1 Yohana 5:19-20.

19 Twajua kuwa sisi tu wa Mungu, na dunia yote hukaa katika yule mwovu.

20 Nasi twajua ya kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue aliye wa Kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa Kweli, yaani ndani ya Mwana wake, Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa Kweli na Uzima wa milele.

Musa naye Eliya walionekana katika lile wingu. Hili laonyesha kuwa Torati na Manabii wote walikuwa mashahidi wa hili kusanyiko la Mbingu, wala sio wa mipangilio na miundo ya kidini tuionayo ulimwenguni tulio sasa. Kama unachokisikia kila wakati hakishuhudii kuwa sehemu yako ipo katika lile kusanyiko la wingu, basi dini yako ni tupu na imekwisha kufa.

Kufikia utimilifu wa kusanyiko hili la kiungu, nia zetu lazima ziweze kukwea na kupaa juu zikayaache ya mwili na damu na kuyaingilia ya kimbingu. Hii yaashiriwa naye Yesu aliposafiri safari ya siku tatu ili akifikie kilele cha ule mlima pamoja na wafuasi wake. Wale ambao wangependa kuuonja uzuri wa Uwepo itawabidi wapae katika Nia yake Kristo kutumia mabawa yake Roho.

Yesu yule yule aliyeomba akisema, "Baba, nitukuze mimi kwa UTUKUFU WAKO, Utukufu ule niliokuwa nao kabla ya misingi ya ulimwengu", alinyakuliwa katika lile wingu la Utukufu alipokuwa akimalizia huduma yake duniani ili kuonyesha ramani ya kutukuzwa wale walioitwa kushiriki katika Utukufu wake Baba. Ili maneno yake yatimie aliposema, "Narudi kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu", Yesu aliingia katika lile wingu la Utukufu na kufanyika Mmoja naye Baba. Lile wingu ni dhihirisho la Utukufu wake Mungu. Mwanadamu awaye yeyote aliye na upambanuzi haswa atajua kuwa faraja yake na kuzawadiwa kwake kuko katika hili wingu la Utukufu. Watu wote walitoka katika hili wingu la Utukufu na WOTE LAZIMA WARUDI KULE. Hii ni kwa sababu hili wingu linaashiria Chanzo na Hatima ya KILA KITU.

Wingu hili la Utukufu lasimamia kusanyiko la kimbingu la watakatifu katika Bwana. Katika kusanyiko hili, Bwana yupo. Lilipo kusanyiko hili, Bwana yu kati yao. Wao na Bwana ni Mmoja na hawawezi kutenganishwa. Kwa mifano na mafumbo, Roho afunua mwelekeo huu tena na tena haswa wakati Musa alipowaongoza wana wa Israeli kutoka Misri kupitia jangwa ili kuingia nchi ya ahadi. Mungu alijifunua kati mwao haswa kupitia wingu mchana kwa kusudi moja la kuwaelimisha na kuwakumbusha watakatifu kuhusu kuungamana waliokuwa nao naye Mungu kabla ya misingi ya ulimwengu. Na kama vile wana wa Israeli walivyobatizwa katika lile wingu, kwa njia ile ile awaye yeyote yule asikiaye na kumakinika katika Kweli, hubatizwa yeye pia katika wingu ijapokuwa ni lile wingu haswa lisiloonekana la Utuku wake Mungu.

Yasikie maneno yake Mtume Paulo, "Tutanyakuliwa panoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa na Bwana pamoja milele. Basi farijianeni kwa maneno hayo". Bwana Asifiwe!!

Elewa hivi...Kule kunyakuliwa katika mawingu ni kule kunakoitwa katika maandiko mengine KUFUFULIWA KWA WAFU. Watanyakuliwa kurudi tena kuungamanika nao Mwili wa Bwana, kwa sababu kuungamanika kwetu hakika ni kwa kiungu katika Bwana. Yote haya hufanyika katika nia zetu wale wanaousikia mwito wake Bwana kupitia Mwili wake wa Wajumbe au Mitume au kwa maneno mengine, Malaika Mkuu.

Usikawahitarajia kuyaona haya yakionyeshwa kwenye runinga na stesheni maarufu ama kupitia redio. Hili ni jambo litendekalo vilindini mwako wewe binafsi na kuendelea hata milele. Mambo ya kiungu huwa na yataendelea kufichwa kutokana na ujuzi wa maarifa ya kiwanadamu, na kupitia kufichwa huku, ulimwengu umeshindwa kuelewa kufunuliwa Kwake. Wanadamu bado hawajaelewa Ukweli wa Milki yake Mungu isiyoonekana inayofunuliwa hata wakati huu tulio. Haigharimu tena ishara kwenye mbingu kama ilivyokuwa zama zile. Leo hii, mwito wetu wa kusanyiko sio kwa mlima fulani uliozungukwa ma mawingu kama ilivyokuwa siku yake Musa wakati wana wa Israeli walipotembea katika mafumbo na vivuli, badala ya kutembea Nuruni ya Kweli ambayo ni Sayuni, makao yake Mungu Baba milele. Kilicho cha Mungu haswa hakionekani kwa mwili na nyama lakini chadumu milele.

Kaisome mistari hii kwa umakini na ukaelewe alichofundisha Roho kupitia waraka wake Mtume Paulo:

Waebrania 12:18-23.

18 MAANA HAMKUFIKILIA MLIMA UWEZAO KUGUSWA, ULIOWAKA MOTO, WALA WINGU JEUSI, NA GIZA NA TUFANI.

19 NA MLIO WA BARAGUMU, NA SAUTI YA MANENO; ambayo wale waliyoisikia walisihi wasiambiwe neno lo lote lingine.

20 maana hawakuwezastahimili neno lile lililoamriwa. Hata mnyama akiugusa huo mlima alipigwa kwa mawe.

21 Na hayo yaliyoonekana jinsi yalivyokuwa ya kutisha, hata Musa akasema, Nimeshikwa na hofu na kutetemeka.

22 BALI NINYI MMEUFIKILIA MLIMA SAYUNI, na MJI WA MUNGU ALIYE HAI, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,

23 mkutano mkuu wa kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika.

Yashike haya kutoka katika hii mistari:

1. Siku tulizo, Mungu hawakusanyi watu kwa mlima wowote uonekanao kwa macho, na ulio na miali ya moto na giza na moshi kama tufani. Hawakusanyi watu kenye kelele za tarumbeta kama ilivyokuwa kule Sinai. Kukusanywa kwetu hakutambuliki kwa macho ya mwili...ni hali ya kiroho. Ni kukusanyika kunakofanyika pasipoonekana kwa macho ya mwili kwa wanaoisikia sauti yake Roho siku hii.

2. Kukusanywa kwa mkutano huu ni kweli iliyoko kwa wale wanaowezatambua hili kwa sasa, wala sio tukio lijalo wakati fulani wa siku za usoni utakaoashiriwa na ishara fulani huko nje. Kama Paulo asema kuwa yeye alifikilia lile kutano kwenye lile wingu la Utukufu Mlimani Sayuni, inastaajabisha vile wanadamu wazitafuta ishara ambazo wanasema zitatukia siku zijazo usoni. Mtu awaye yeyote yule anaweza kupaa wakati wowote ule, hata sasa hivi asikiapo sauti ya tarumbeta (ujumbe wake Bwana).

Na Ujumbe huu wa tarumbeta wasema nini? Ujumbe ni kuwa kuna mwito wa kukusanyika kwake Mungu katika lile wingu la Utukufu Mlimani Sayuni.

Hili hufanyika mwanadamu anapoisikia Sauti ya Roho wa Bwana iitwayo TARUMBETA katika maandiko ya biblia. Ni Sauti ya Roho inayowakutanisha watu kwake Yeye. Kumbuka kuwa Bwana Mwenyewe ndiye Ile Roho (2 Wakorintho 3:17).

Wakati Mtume Paulo alipoandika waraka wake maarufu kwa ndugu Wathesalonike akizungumzia kile wengi wanachokiita KUTOWEKA, alijaribu kuwakumbusha upya na kuwahimiza waliokuwa wamechoka tayari, kuhusu Tumaini La Mwito wao. Kutoka ule waraka ni dhahiri kuwa Mtume Paulo alikuwa anawazungumzia mambo ambayo walikuwa wameyajadili pale mbele wakiwa naye. Huu ulikuwa ni waraka kwao ndugu wenye imani kama yake Mtume na walioelewa lugha aliyokuwa anazungumza kupitia ushirika waliokuwa nao hapo mbeleni. Hakuna Mthesalonike wa kawaida angeelewa ayasemayo Mtume Paulo kama hangekuwa ametiwa Nuru ya hekima ya kimbingu.

Tangu siku ile Injili ilihubiriwa, Mbingu Mpya na Nchi Mpya zimefunuliwa machoni pao wanadamu, na wanaofuatilia wakaimiliki hii Milki Mpya katika Kristo wanena kwa ndimi mpya, usemi mpya, kwa maneno mengine. Katika maono ya wale Mia Na Arobaini Na Nne Elfu, waliokombolewa duniani na kusafirishwa hadi vileleni mwa Mlima Sayuni, hili ni dhahiri. Hawa wanalo jina la Baba vipajani mwa nyuso zao na wanena kwa ndimi au lugha ambayo hakuna yeyote duniani aielewa. Yamaanisha kuwa wao wana nia mpya na mawazo mapya...yake Babao...na wanena lugha yake Mungu..ambayo ndiyo pia Lugha Ya Roho.

Hili latendeka sasa hivi wanaposadiki wale wanaoamshwa na ule Mwito, kwa kuwa wameufikilia Mlima Sayuni, Yerusalemu ya kimbingu, Ulimwengu ambao wakusanya kila kitu kwake Mungu. Lugha wanayoongea nayo hawa roho waliokombolewa haiwezi kamwe eleweka kwa akili za walio wa mwili na nyama. Twaonywa kuwa tusikawahitarajia anayefikiri kupitia kwa maarifa ya mwanadamu atapokea taarifa itokanayo na watakatifu walio katika Nuru. Kwake yeye taarifa ya Roho ni upumbavu.

Fikiria kwa makini, Yesu aliyazungumzia mambo ya Ufalme kwa ndimi za Roho na mambo haya aliyoyanena yalionekana na wingi wa umati kama hekaya na mafumbo tu. Lugha yake ambayo kwa undani wake twaielewa ilileta majibizano mengi na mvutano, na kwa kweli haikueleweka hata kwa wale waliokuwa makuhani wakuu wa dini siku zile. Wakati Nikodemo alipomuuliza Yesu, "mtu mzima awezaje ingia tena tumboni mwa mamake na azaliwe tena..." kwa kustaajabishwa na lile swali, Yesu alimuuliza "mwalimu mkuu kama wewe Israeli na kweli ndogo kama hii hauielewi.." Hili linaendelea katika dini tofauti tofauti ulimwenguni hata wa leo. Watu wengi hawaielewi taarifa ya Roho kuhusu tumaini la dhamani la Imani waliyoitiwa wala hawaioni njia panda iliyowekwa mbele yao wazi kuwapeleka Uzimani.

Lakini kati ya haya yote kulikuwa na kundi dogo lisilo na sifa zozote ambalo macho yao ya ndani yalifunguliwa wazi kuona kikamilifu na kuielewa taarifa yake Yesu. Na hiyo ni kweli hata sasa. Baadaye Yesu aliwaelezea waliotafuta upambanuzi zaidi kwa nini ilimpasa Masihi aseme kwa mafumbo katikati ya umati, lakini awafafanulie zaidi waliomsaka sirini na awaelezee mambo bayana. Yesu alijibu virahisi na kusema, "Kwa walio nje - yaani walio gizani, yote yapeanwa kwao kwa mafumbo. Heri kwenu kundi dogo mwayaona na kuyasikia yaliyowapita wa kale na watawala wa kizazi hiki".

Yesu yule yule ndiye anayezungumza kupitia Roho katikati ya watu wake walio na masikio ya kusikia. Kwa hivyo wanadamu wanapaswa kuwa makini ili kutambua nyakati na mambo wanayoyasikia ili wawe waridhi wa wokovu huu mkuu unaofunuliwa sasa. Wanadamu wanafaa kuwa makini wasifuate njia walizofuata wale waliomsulubu Yesu kwa upumbavu wao. Kama mwivi gizani usiku, mjumbe wake Mungu huja na kuwahabaria walio na masikio ya kusikia siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kama tujuavyo, wengi huukataa.

Shida ya mwanadamu ni kuwa amekosa kusikia. Na kiroho ni kama aliyekufaganzi. Hauelewi Utukufu wake unaoambatana na mambo yasiyoonekana ya Ufalme wake Mungu. Mpango kamili wa ukombozi, ambao pia waitwa Urejesho Wa Kila Kitu ni kumtambulisha kila mwanadamu kwa ule Utukufu alioupoteza uliopo ndani yake Mungu. Tangu siku zile Neema hii iletayo wokovu ilipotangazwa na kudhihirishwa kutoka mbinguni, Baba anena kuhusu kwa usemi ulio sawa kuhusu wokovu huu uliowekwa wazi kwa kila mwanadamu. Baba hatazungumza tena katika mafumbo na kwa mifano vivuli kama alivyonena zama zao Musa na za manabii. Kila mtu na akatulie na kuisikiliza Sauti iwaongozao wanakondoo kurejea zizini mwao. Hata Musa aliyekuwa mtumishi mwaminifu katika mambo msingi aliyoyapokea, alitangaza kupitia Roho kuwa Baba atamwinua mwanadamu duniani, naye ndiye mtakayemsikia.

Kumbukumbu LaTorati 18:15, 18.

15 Bwana Mungu wako atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; MSIKIZENI YEYE...

18 Mimi nitawaondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe, nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.

Miaka mingi baadaye, Mungu angetia dhibitisho Lake La Kibali kwake Yesu alipoguruma toka mbinguni alipotangaza, "Huyu ndiye Mwanangu pekee niliyependezwa naye, MSIKIENI YEYE". Twanenewa na yale yale kupitia Roho...ambaye ndiye Upako ulio ndani, lakini wengi kwa kutoelewa wamening'inia kushukilia sauti ya Musa na kukosa kuisikia Yake aliyetiliwa Muhuli wa Kibali Wake Mungu.

Wakati uliopita, tuliyasikia mambo kimafumbo tu, na kwa njia ya kuashiria, basi ikatulazimu kutembea kama walio gizani na kujiundia matumaini yasiyoafikiana na mbinu za kidini za kujaribu kumfurahisha Mungu aliye na hasira zisizotulizika. Lipi ambalo wanadamu hawajawahifanya kujaribu kumtuliza Mungu na kuingia vitabu vyake vyema (kama anavyo), kwa ajili ya vile tulivyomwona Mungu? Damu za kafara za watu na wanyama, mahema na mahali wakfu pa kuabudia, mipangilio ya kuabudu, vuvio huku na kule, mikutano ya mahema, mikesha, mavazi fulani, ibaada za batizo, matoleo tofauti tofauti, tohara sio haba, kustahimilisha miili uchungu, kutokula na mifungo tofauti tofauti, njia tofauti za kuomba na kutafakari n.k.

Mwanzo mwanzo, njia hizi zake mwanadamu alizozivumbua yeye zilionekana kana kwamba zilimwelekeza mahali fulani mpaka alipovumbua kuwa alikuwa anakimbilia tu mzunguko duara akiwa amefunga macho, akidhani kuwa yumo safarini. Macho yako yalipofunguliwa ulitambua kuwa hukuwa umesogea hata hatua moja, ilhali ulikuwa umechoka sana. Kuhamia makanisa tofauti au kuwatafuta wachungaji watakaokulisha ilionekana kama yatenda kazi, lakini baadaye ukajua haikutenda lolote. Ukombozi wa kweli na kutosheka hakukuwadia..safari za kutafuta hili na lile hazikwisha. Safari zilizoelekea kukosa tumaini zaidi...shimo la giza, kwa maneno mengine.

Kwa kutumia maneno yake Mtume Paulo, hawa ni wale wasomao lakini wasije kuutambua Ukweli. Haya ni yale mawazo yazungukayo kwa mviringo usioisha wa kidini. Manabii wa kale wa Waazeki na Wamisri walisikia lakini kwa kivuli tu na wakajenga minara mikuu ya pembe tatu wakijaribu kuufikia Uungu, ingawa baadaye walitambua kazi zao zilivyokuwa nyonge. Vile vile wayahudi walijenga hekalu lililokuwa la kushangaza sana zama zile. Walitenda hili wakidhani pengine kupitia hili wangepata kukaribiana naye Mungu. Hasira iliwajaa Alipokuja Yesu na kusema "Mimi Ndimi Hekalu". Wafuasi wake wakaja baadaye na kukiri, "Sisi ni Hekalu Lake Mungu".

Bila kutambulika na wengi, hizi itikadi zimefurika na kujaza kila mfumo wa dini leo. Haya ni mafuriko yaliyojaa uongo uliozificha funguo za maarifa kutoka kwa wengi watafutao Ukweli. Uongo huu huisha wakati mwanadamu anapoanza kuisikiliza Sauti Yake Roho. Kusikiliza ni kama kupokea ule Ufunguo Wa Daudi ufunguao malango ya jela za kifo na mauti. Kwa kuisikia kweli tena, nafsi kama ndege hupata mwanya wa kutorokea kutoka kwa mtego wake mnasaji na kuingia kwenye uhuru mtukufu wao (M)wana wake Mungu...Huru tokana na dhambi...huru tokana na hofu na kifo.

Wanadamu wataelewa lini matamshi yake Yesu, "Mimi Ndiye Ufufuo", "Mimi Ndimi Uzima", "Mimi Ndiye Mwanzo", "Mimi Ndiye Mwisho", "Mimi Ndiye"? Unaelewa huu msemo, "Uzima Umewadia"? Ni wakati mwafaka wake mwanadamu kuwacha wazo lake Matha aliyekuwa amekolezewa kasumba ya imani fulani kuwa kuna ufufuo wa kimwili utakaofanyika kule nje wakati fulani ujao. Wakati Yesu alipouliza swali, "Waamini nduguyo Lazaro atafufuka tena?" Matha alijibu, "Ndio naamini atafufuka tena siku ile ya ufufuo". Dadake huyu Lazaro kama watu wengi wa kizazi hiki aonyesha fikra za wengi ambao waamini kuwa kunayo siku ambayo waliokufa watafufuliwa na kuingia utukufuni. Wakati umewadia na ndio huu tulio wa kuisikia Sauti yake Baba ikiongea kupitia mdomoni mwake Yesu na kutangaza kuwa hakuna tukio kama hilo lijalo siku fulani ya usoni, bali asema, "Mimi ndimi ufunuo na Uzima wa milele".  Sauti hiyo isahihishayo yake Yesu ilikuwa ilifukuze pepo la upumbavu na kutoamini kutoka kwa kila mwanadamu atakayenyenyekea na kusikiliza.

Leo hii ule Uzima ni dhahiri kwa kila mtu kuona. Mwanadamu anahitajika kusikia kwanza, halafu kuutambua Uhai huu Mmoja. Ni kuutambua huu Uhai kama Uzima wako na kwa imani kuamka na kurejea katika Uzima huu. Mwanadamu akikosa kusikia, yeye huikataa Neema impayo wokovu, na huendelea katika safari yake ya mviringo wa utupu. Kwa sababu hii, tunawasihi kuwa ikiwa bado leo, ukiisiia ile Sauti dhahiri, tusiifanye mioyo yetu kuwa migumu na kufa katika kutoamini kama walivyo wengi wa umati kule nje. Jiambatanishe na Sauti ya Ukweli na ukaingie katika pumziko lako la Utukufu.

Usijisumbue kutafuta ishara na maajabu ya nje, wala kugaagaa jangwani ukidhani kuna msaada kule. Usitazame Mashariki ya Kati ukitumaini kuna kitu kitatendeka kule, ama unabii fulani, zote hizi zitakutoa kutoka kilicho kweli. Usidanganywe na vitabu vilivyoandikwa na mababe wa fani za masomo wa siku hizi, kwa sababu kile tu watakachokifanya ni kukuondoa kwenye kweli iliyo na uwezo wa kuiokoa nafsi yako. Unachohitaji ili kukusafirisha nafsi yako iliyo kama ndege kurejea Shambani mwa Bwana ni kuisikiliza Kweli. Kile Baba anachoweza na atakachofanya ni kutangaza Ukweli uliofichika kutoka kwa ufahamu wake mwanadamu tangu misingi ya ulimwengu. Hili laleta uamsho kwa wana wa Mungu ambao wamekufa na kuzikika katika hali ongo ya mwili na damu wakitengeka katika mawazo yao kutoka kwa Uzima tele upatikanao ndani Mwake Roho.

Kama Lazaro, kila mtu atahitajika kukubali jiwe lililo moyoni mwake lisukumwe na liondolewe ili akaweze kusikia Sauti yake Baba ikisema, 'Mwanangu, Toka kaburini'". Hilo jiwe lawezakuwa ni imani unazozituza ulizojiwekea kama hazima ya kiungu ama iwe ni itikadi na tamaduni za jadi za wanadamu ambazo hukufanya ujihisi u mmoja na wengine katika mipango yao bila kujiona katika mpango wake Mungu. Yaache haya yaende na utamsikia Baba akizungumza, na sio tena kwa mafumbo. Kama wangoja kama Matha kuwe na tukio fulani siku ya usoni, wewe umefungiwa kaburini ukitembea katika nuru fulani ambayo kwa hakika ni giza.

Wakati vikwazo vimfanyavyo mwanadamu kutosikia vinaondolewa, anasikia mlio mkuu unaoleta ukumbusho wa mambo aliyoyasahau. Mambo kuhusu mahali pake pamoja na nyota za asubuhi na kuutambua Ukweli kuwa Yeye Ndiye. Kweli Kuu hung'aa tena, naye hufunguliwa kutoka vifungo vilivyomtia pingu maishani ya mwili na damu. Kuitambua na kuielewa ile Kweli ndiko kunakoleta uponyaji na ukamilifu wa watakatifu. Hadi sasa, ishara za nje zinazoambatana na mitazamo ya vitu vilivyoko nje hazijanawirisha maisha ya wanadamu hata chembe, na hata hazijawavuta wao hata hatua moja kuusogea Ufalme wa Mungu. Kama hizi ishara zingekuwa ndizo, wana wa Israeli waliyoyaona makuu kupitia mkono wake Musa wangeingia uzimani, lakini haikuwa vile. Hata makusanyiko waliyomfuata Yesu hawangenufaika na kupokea cha Kweli kwa sababu hawakulenga kushika habari ambazo Yesu alipeperusha.

Cha maana kilikuwa ni kuisikia Kweli, na kwa sababu hiyo, maneno haya, "Tilia maanani unavyosikia kile Roho anachosema na kanisa" yaenda tena na tena kwa wote wakao ulimwenguni huu. Sauti ya Roho ndio ile Tarumbeta iitanayo ikiwatafuta wana wake Mungu waliolala ili kuwaamsha na kuwarejesha na kuwahifadhi kwenye Utukufu wake Baba. Hii Sauti yasambazwa kupitia mwili wa wajumbe na watenda kazi (au Malaika Mkuu) ambao wameungana kwa kusudi moja na Bwana kueneza Sauti hii ya Roho kwa wanadamu wote.

Wanapoisikia Sauti hii, au mlio huu, au tarumbeta hii, siri yake Mungu inakamilika, na ule msemo usemao, "...na wote watanijua kutoka aliye mdogo hadi aliye mkuu..." unatimilika. Na huu ndio Mwisho. Wanadamu wote pale hatima watapambanukiwa kuwa walichokiwaza kumhusu Mungu kilikuwa tu ni fundo la moshi wa mawazo yao yatokanayo na moyo uliotiwa giza. Katika Uamsho, mwanadamu huanza tena kutembea na kuishikilia nafsi yake ikiwa ndani yake Mungu.

Yesu aliliweka hili dhahiri aliposema, "Kumjua Mungu na Mwanawe uliyemtuma ni Uzima wa milele"  (Yohana 17:3). Maarifa haya yamepita maneno tu na kuyapita mawazo duni kumhusu Yesu aliyezaliwa na mwanamke fulani. Inakubidi uwezeshwe kuona kwa undani ili kuelewa hili. Kama kifurushi kilivyo, maarifa ya Mungu na Mwanawe huambatana moja kwa moja. Ukimpata Mmoja hata yule mwingine itakubidi uwe Naye. Kujua wanavyojumlishwa ndio Uzima wa milele. Kumjua Baba ni lazima umjue Mwana, na Mwana sio mwingine ila ni Kristo aliye ndani mwako. Kwa kweli hakuna awezaye kumjua Mungu bila kujijua yeye mwenyewe...Mwana Katika Kweli. Kupitia ufunuo huu toka juu, anayedanganya, ambaye ni Shetani, anafungwa na minyororo na huangushwa kama radi na kuingia kwenye shimo la giza kumaanisha kuwa hatakuadhiri tena milele.

Huu Ukweli wa kiungu uliofichwa katika chombo hiki cha udongo ndio njia pekee kuelekea kwake Mungu, kwa kuwa Yeye Ni Mmoja na Baba. Katika hali yake halali ya kukwezwa na uamsho, yeye ndiye Baba, Mungu Aliyefichika ndani ya mwili wa damu na nyama wa mwanadamu wa ulimwengu huu. Jina 'Ulimwengu' lamaanisha upumbavu wa kutoielewa siri yake Mungu na yake Mwanadamu. Lakini Ulimwengu huu huisha wakati mwanadamu huamka na kutambua kuwa yeye ni kiungo katika Mwili wake Mungu. Mwanadamu ni dhihirisho duniani Lake Mungu asiyeonekana. Haya ndiyo maarifa yanayotangazwa na ile Tarumbeta inayomwinua mwanadamu hadi hatima ya Kweli kuwa yeye ni mmoja na Mungu asiyegawanyika na asiye na uharibifu.

Ukweli huu huzivunja nira za tamaa na humwamsha mwanadamu katika tabia asili ya Mungu aishiye ndani mwake. Yeye hutambua kuwa hakuzaliwa kupitia mwili na damu, na kuwa uhai wake ni wa kutoka milele, kabla ya kudhihirika hapa uliwenguni huu tuuonao kwa macho. Yeye hukumbuka kuwa ni Mmoja na Muumba wake na sio mmoja na kilichoumbwa, na kwa lile yeye hutiwa nguvu ya kuvishinda vyote akutanavyo navyo katika ulimwengu huu wa mambo yapitayo.

Katika Uamsho huu, mwanadamu hukusanywa na kurejeshwa katika kusanyiko la kimbingu la roho zilizokamilika katika Mungu na huimba katika kutaniko la Mwenye Nguvu pamoja na Sauti za maji mengi wakisema, "Dhambi, wapi uchungu wako? Mauti, wapi ushindi wako?" Sauti ya maji mengi inayorudirudiwa katika kitabu cha Ufunuo ni kusanyiko lile la watakatifu katika lile wingu la Utukufu. Lile wingu ni unyevu unyevu wa maji yaliyotiwa Uhai yaliyokusanyika na kupaa kwake Mungu na huishi kwa ajili yake Mungu na huongea kwa Sauti yake Mungu. Wao huongea pamoja kama ngurumo kuu, na ndio maana waitwa Wana Wa Ngurumo.

Sauti ile ya maji mengi ndiyo ile ile iliyotembea (yaani kushiriki) katika shamba la Edeni. Katika uasi, huu ushirika ndio Adamu alioupoteza. Katika hali yake ya chini ya uasi, Adamu hangeweza tena sikia na akasahau mahali aliposhuka kutoka, kati ya miili ya kiungu na Utukufu wa lile wingu. Akazisahau nyimbo za Sayuni zilizotangaza, "Mimi ndiye niishiye, na kando Yangu hamna mwengine". Akasahau kuutafakari Uhai wa Muumba wake. Na basi akapoteza nguvu za kushinda mauti.

 

Yohana 14:26.

26 Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.

Bwana asifiwe. Tarumbeta au Sauti ya Roho ii hapa kutukumbusha tuliyoyasahau katika kaburi la usingizi wake Adamu. Roho wake Mungu kama umande uiloweshayo ardhi na pumzi yake Mungu kupitia Tarumbeta zile, zatia Uhai ndani mwake mwanadamu kupitia kukumbuka kumrejesha katika utukufu wa Milki ya Edeni. Kwa kukumbuka, mwanadamu akwea tena na kurudi kwenye wingu la Utukufu na kujijua tena kati ya miili ya kimbingu ambazo ni zile nyota za asubuhi.

Leo Mwito umetoka wa kumtoa Adamu kutoka mavumbini ya mauti na kaburi na kumuungamanisha tena katika ushirika mtamu wa kusanyiko la ulimwengu mzima katika lile wingu. Bwana Mmoja, Mwili Mmoja, Roho Mmoja, Mungu Mmoja na Baba Mmoja Amefunuliwa na kukusanywa kwetu ni Kwake Huyu Mmoja.

Amka...Amka na ukajitikise toka kwenye mavumbi, ukajivike mawazo ya Roho na ukaungamanike na Bwana. Yaanza kwanza kwa kusikia halafu kujinyenyekeza kwenye Kweli hii kwa kukiri. Mawazo yetu lazima yaambatanishwe tena na yake Bwana ili kutembea na kunena kama yeye kwa sababu Yeye ndiye ule Uhai. Jitambue wewe kama Yeye Aliye Juu, na kwa imani ukachukue nafasi yako katikati ya mashahidi wengi katika lile wingu. Ukajifunze kuongea na Sauti ya maji mengi kati ya yale mawingu yanayokiri Jina La Bwana.

Ile pazia imeharibiwa milele na mlango uliofunguka kuwekwa wazi mbele ya kila mwanadamu ili aingie ndani na kushiriki katika Ushirika wa Upendo na furaha katika wingu la Utukufu. Roho asema na kila mwanadamu PANDAA HATA HAPA JUU.

Baraka.

Trevor Eghagha.